MKUTANO MAALUMU WA SACCOS YA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE WAFANYIKA LEO
Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kampasi ya Kivukoni ( KIVUKONI SACCOS LTD) leo kimefanya Mkutano Mkuu Maalumu wa Kumkaribisha mlezi wa Chama hicho ambaye ni Mkuu wa Chuo Prof. Shadrack Mwakalila. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo kwenye mkutano huo Kaimu Naibu Mkuu wa Chuo Utawala, Fedha na Mipango Bi. Ukende Mkumbo amewataka Wananchama wa Chama hicho kujiimarisha katika kusimamia Chama na kuhakikisha wanachama waliokopa wanarejesha mikopo. Bi Ukende amesema dhamana ya kurejesha mkopo ni ... a Mwanachama husika, lakini dhamana ya kusimamia Chama ni ya Wanachama wote. Wanachama wametakiwa kuzingatia taratibu na Sheria za kukopa ili kuepusha usumbufu miongoni mwa Wanachama. Kupitia Mkutano huo Maalumu wa Wanachama wa KIVUKONI SACCOS LTD walipitisha Sera, Miongozo na Kanuni mbalimbali za namna ya Mwanachama anavyoweza kupata mkopo wa Nipige Tafu, Mkopo wa Sikukuu, Mkopo Mdogo,Mkopo wa dharura na Mkopo wa Maendeleo. Imetolewa na: KITENGO CHA HABARI NA MASOKO CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE 10.01.2023 Read more >
[ 2023-01-11 ]
Visitors Counter
Flag Counter
Collaboration

TCU Link

NACTE Link
NECTA Link
ZHELB Link
HELSB Link
MoEST Link
MoEZ Link
Social Networks
Facebook
Instagram
Youtube
Twitter
Contact us
Hotline : +255 (22) 2820041/47
P.O.BOX : 9193 Dar es Salaam,TANZANIA
Email : rector@mnma.ac.tz
Location : Kivukoni Dar-es-salaam