PROFESA MWAKALILA ASISITIZA UADILIFU, UAMINIFU NA UZALENDO KWA VIONGOZI WA WANAFUNZI
Mkuu wa Chuo cha KumbuKumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Shadrack Mwakalila amewapongeza viongozi wapya wa serikali ya Wanafunzi (MASO) kwa kuaminiwa na Kuchaguliwa Kuwa viongozi kwa mwaka 2023/24 ambapo amewataka viongozi hao kutumia vizuri fursa hiyo. Prof. Mwakalila amesema hayo leo wakati wa Semina elekezi ya kuwajengea uwezo viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi huku akiwataka viongozi hao kuwa mfano wa kuigwa kwa kuhakikisha wanasoma kwa juhudi na Maarifa na kufanya vizuri katika Mitihani. Mkuu huyo wa Chuo pia amewata Viongozi hao wa ... Wanafunzi kuwa Waadilifu,Waaninifu na Wazalendo kwa Chuo na Taifa kwa ujumla, pamoja na kuhakikisha ada zinalipwa kwa wakati. Prof. Mwakalila pia amewataka Viongozi hao wa Wanafunzi kujiepusha na udanganyifu wa aina yeyote katika Mitihani na kujiepusha na Makundi ya Uchochezi. " Nasisitiza suala la kuheshimu Wafanyakazi wote, Walimu na Waendeshaji lakini Muwaheshimu na Wanafunzi wenzenu pia,"alisiaitiza Prof. Mwakalila. Amewataka Wanafunzi kuhakikisha wanatumia vizuri mitandao ya kijamii kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ya kimasomo na si vinginevyo. Imetolewa na; Kitengo Cha Habari na Masoko CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE 19.06.2023 Read more >
[ 2023-06-20 ]
Visitors Counter
Flag Counter
Collaboration

TCU Link

NACTE Link
NECTA Link
ZHELB Link
HELSB Link
MoEST Link
MoEZ Link
Social Networks
Facebook
Instagram
Youtube
Twitter
Contact us
Hotline : +255 (22) 2820041/47
P.O.BOX : 9193 Dar es Salaam,TANZANIA
Email : rector@mnma.ac.tz
Location : Kivukoni Dar-es-salaam