|
|
|
VIONGOZI WAPYA SERIKALI YA WANAFUNZI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA, KANUNI NA MAADILI YA UONGOZI
Naibu Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere anayesimamia Mipango, Fedha na Utawala, Prof. Evaristo Haulle amewataka viongozi wapya wa serikali ya wanafunzi – MASO kutambua kuwa uongozi ni dhamana ambapo amewasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za chuo.
Kauli hiyo ya Prof. Haulle ameitoa leo wakati akifungua semina elekezi ya kuwajengea uwezo viongozi hao wa serikali ya wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2026/27.
Prof. Haulle amewataka Viongozi waliochaguliwa kuwa Uongozi ni shamans ambayo wamep ...
wa na Wanafunzi wenzao hivyo ni lazima watambue nafasi walizopewa kwa kuwa mfano wa kuigwa na kuhakikisha Nidhamu na Maadili mema katika uongozi.
Prof. Haulle aliongeza kuwa pamoja na nafasi za uongozi walizonazo, wanapaswa kuzingatia masomo ambayo ndiyo msingi wa wao kuwepo Chuoni.
Naibu Mkuu huyo wa Chuo aliwaasa viongozi hao kuhakikisha wanajiridhisha na usahihi wa taarifa ambazo wanazipokea kabla ya kusambaza kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.
Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano na Masoko
Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere
2.07.2026
Read more >
[ 2026-07-04 ]
|
|
|
|