KAZI ZA CHUO

 

  • Kutoa vifaa vya masomo na programu za mafunzo katika sayansi ya jamii, uongozi na elimu endelevu na Sayansi shirikishi;

  • Kushiriki katika utafiti na maendeleo katika taaluma zilizoainishwa katika aya ya (a) na kutathmini matokeo yaliyopatikana kupitia programu za mafunzo ya Chuo hicho;

  • Kutoa huduma za ushauri kwa umma na sekta binafsi katika nyanja maalumu kama ilivyoainishwa katika Sheria Namba 6 ya 2005;

  • Kudhamini, kupanga, kuwezesha na kutoa vifaa vya mikutano, makongamano, semina na warsha za majadiliano ya mambo yanayohusu sayansi ya jamii, uongozi na elimu endelevu;

  • Kufanya mitihani na kutunuku tunzo za Chuo kama ilivyoidhinishwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi.

  • Kupanga shughuli za uchapishaji na usambazaji wa jumla wa vifaa vinavyozalishwa kutokana na kazi na shughuli za Chuo.

  • Kushiriki katika shughuli za kuongeza kipato kwa ufanisi na kukuza ujasiriamali.

  • Kuanzisha na kukuza ushirikiano wa karibu na Vyuo Vikuu na taasisi nyingine za elimu ya juu na kukuza ushirikiano wa kimataifa na taasisi zinazofanana kimalengo na chuo.

  • Kufanya shughuli na miamala yote kama ilivyopendekezwa na Bodi ya Uongozi au suala muhimu kwa utekelezaji mzuri wa majukumu ya Chuo.

  • Kufanya kazi nyingine ambazo Waziri au Bodi ya Uongozi inaweza kuelekeza kwa Chuo, au kama ilivyo kawaida au inayofaa kwa maslahi ya Chuo au kazi nyingine zilizopo.
     

Idadi ya Waliovinjari
Flag Counter
Washirika

TCU

NACTE
NECTA
ZHELB
HELSB
MoEST
MoEZ
Mitandao ya kijamii
Facebook
Instagram
Youtube
Twitter
Wasiliana Nasi
Simu : +255 (22) 2820041/47
S.L.P : 9193 Dar es Salaam,TANZANIA
Barua Pepe : rector@mnma.ac.tz
Mahali : Kivukoni Dar-es-salaam