KUHUSU UTAFITI


Utafiti
Ushauri
Jarida
        UTAFITI

Utafiti na Ushauri wa kitaalamu ni moja ya Vitengo katika Chuo ambapo kitengo hiki kinashughulikia huduma za Utafiti na Ushauri wa kitaalamu kwa jamii. Kitengo kilianzishwa kwa lengo la kuendesha na kuratibu shughuli za utafiti na kuwezesha kubadilishana maarifa. Shughuli za utafiti hufanywa kwa njia ya kimfumo inayolenga kushirikisha Chuo na wadau tofauti wa utafiti kama serikali, viwanda, Asasi zisizo za kiserikali, kampuni za madini na mafuta na kampuni za ujenzi ambazo zinakusudia kutumia tafiti kusaidia shughuli zao.
Shughuli za utafiti hufanywa katika vikundi vyenye tajriba mbalimbali kwa kushirikisha idara mbalimbali ambazo ni pamoja na idara ya Sera ya Umma, Masuala ya Jinsia, Uhusiano wa Kimataifa, Utawala Bora, Uchumi na Usimamizi wa Rasilimali watu.
Idara hii ina Jarida moja lililosajiliwa kwa namba ya usajili ISSN 1821 - 6989 na iko kwenye mchakato wa kuzindua Jarida kuwa jarida litakalopatikana la mkondoni.
Tunayo raghba na hamu ya kukuza tafiti zetu kupitia viungo (links) mbalimbali kwa kushirikiana na wasomi wa kimataifa ambao wana mawazo, fikra na mitazamo mipya anuwai.

MAELEZO YA KITENGO CHA UTAFITI NA USHAURI WA KITAALAMU
Chuo kimedhamiria kutoa tafiti za hali ya juu ili ziweze kuleta athari kwa jamii ya kitaifa na ya kimataifa ili kuchochea upatikanaji wa fedha za kuwafadhili washiriki na wanachuo wanaotarajiwa kufanya tafiti za uzamili.


Kitengo cha Utafiti na Ushauri wa kitaaluma kinahakikisha kuwa:
Tafiti zilizofanywa zinakuwa bora zaidi na zinazoweza kutumiwa na wadau wa utafiti katika usimamizi, utekelezaji na tathmini ya mipango yake.
1. Matokeo ya utafiti hutumiwa vizuri katika kutatua na kujibu shida.
2. Tafiti zote hupitiwa na kutathminiwa kufikia viwango vya kidunia na vya kimataifa.
3. Mada za utafiti na maswali ni muhimu na ziko katika vipaumbele vya Chuo.
4. Kuhakikisha zinatumika njia tmbalimbali za kitaaluma katika tafiti zote ili kupata matokeo bora zaidi ya kisayansi.
5. Wanataaluma kutoka fani mbalimbali wanatumia tafiti hizo kuhakikisha wanatoa huduma za Ushauri wa kitaalamu kwa taasisi za serikali na binafsi na ndani na nje ya nchi.

SHABAHA NA MALENGO
Kitengo cha Utafiti na Ushauri wa kitaalamu cha Chuo kinahakikisha kuwa matokeo ya tafiti yanayotokana na tafiti za wataalamu wake yanatumiwa na wadau wa utafiti ikiwamo serikali, viwanda, Asasi za Kiraia na kampuni mbalimbali kuhusu mipango yao, uamuzi, na sera ili kuboresha shughuli zao za kila siku ambazo zinaweza kuleta mabadiliko makubwa nchini.

UPIMAJI WA SHUGHULI ZA UTAFITI
Ili kuhakikisha tafiti zake zinakuwa bora, Chuo kupitia kitengo cha utafiti na ushauri wa kitaalamu kina kawaida kufanya tathimini ya pamoja kwa kufanya majopo anuwai ya wataalamu yenye lengo la kutathmini matokeo ya utafiti uliofanywa na wataalamu wa Chuo yanafikiwa. Tathmini huongozwa na mambo yafuatayo, maudhui yaliyoandikwa kwenye mada, uhalisia wa kazi yenyewe ya utafiti, Mchango maudhui ya Maarifa ya utafiti huo, uhusiano wake katika taaluma, Umuhimu kitaaluma kwa Watu binafsi walioko katika uwanja huo wa Taaluma, Uwasilishaji na Ubora wake kwa jumla.

BODI YA UHARIRI
Chuo kina Bodi ya Wahariri ya kukagua masuala ya maadili na kuhakikisha viwango vya ubora vinazingatiwa na watafiti wakati wa kufanya utafiti na katika mchakato wa uchapishaji pia.
 

Idadi ya Waliovinjari
Flag Counter
Washirika

TCU

NACTE
NECTA
ZHELB
HELSB
MoEST
MoEZ
Mitandao ya kijamii
Facebook
Instagram
Youtube
Twitter
Wasiliana Nasi
Simu : +255 (22) 2820041/47
S.L.P : 9193 Dar es Salaam,TANZANIA
Barua Pepe : rector@mnma.ac.tz
Mahali : Kivukoni Dar-es-salaam