NENO LA UKARIBISHO

Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (CKMN) ni taasisi ya elimu ya juu iliyotokana na Chuo cha Kivukoni kilichoanzishwa mnamo tarehe 29 Julai, 1961. Chuo kina historia ya kuwa taasisi pekee ambayo imehifadhi kumbukumbu muhimu za kuwajengea uwezo viongozi wa umma katika fani ya uongozi na maadili, hususan wakati wa kipindi cha mfumo wa uongozi na utawala wa chama kimoja. Shabaha ya CKMN ni kuhakikisha kwa wakati wote ujifunzaji unafanyika kwa njia zilizo bora kuanzia katika ufundishaji, utafiti, ushauri wa kitaalamu na utumishi wa umma. Lengo ni kuhakikisha kunakuwa na mazingira mazuri ya kujifunzia yenye kulenga kuchagiza utafutaji wa maarifa zaidi, kukuza ubunifu, kukuza fikra kwa utunduizi na ustadi ulio endelevu.

CKMN kina maktaba nzuri. Watumiaji wote wa Maktaba ya CKMN wanapaswa kuzingatia sheria na kanuni za makatba. Shughuli za Maktaba ya CKMN zinalenga kurahisisha shughuli za ufundishaji na utafiti wa Chuo kupitia utoaji wa vitabu, majarida, magazeti na vifaa vingine vya kusoma kwa wahadhiri, wafanyakazi wa utawala, wanachuo na watafiti wengine.

Wanafunzi wana uhuru kamili wa kuabudu, ila uhuru haupaswi kuchupa mipaka na kukera au kuzuia uhuru wa wengine kufurahia kwa namna yoyote ile. Aidha, uhuru huo haupaswi kuzuia shughuli nyingine za CKMN kuendelea. Huduma za kiibada kwa madhehebu yote makubwa hupatikana kwa umbali wa kutembea tu kwa mguu kutoka CKMN.

CKMN kinahimiza wanafunzi kushiriki katika shughuli mbalimbali za michezo na burudani. Huduma za michezo zinazopatikana katika Chuo ni pamoja na uwanja wa mpira wa miguu, uwanja wa mpira wa mikono, uwanja wa mpira wa kikapu na wa mpira wa wavu.

Wanafunzi wanapata huduma za matibabu katika zahanati ya CKMN, ambayo inaongozwa na mtaalamu wa matibabu. Kwa maradhi au shida zote kubwa za kiafya zinazohitaji uangalifu maalumu hupelekwa katika hospitali zinazohusika.

Kwa taarifa zaidi za Chuo peruzi zaidi tovuti hii ili kupata uelewa mzuri zaidi kuhusu CKMN. Ni imani yetu kuwa tovuti hii itakunufaisha zaidi na itakuwa msaada kwako.
Asanteni sana na karibuni Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere

Prof Shadrack S. Mwakalila

Mkuu wa Chuo

 

Idadi ya Waliovinjari
Flag Counter
Washirika

TCU

NACTE
NECTA
ZHELB
HELSB
MoEST
MoEZ
Mitandao ya kijamii
Facebook
Instagram
Youtube
Twitter
Wasiliana Nasi
Simu : +255 (22) 2820041/47
S.L.P : 9193 Dar es Salaam,TANZANIA
Barua Pepe : rector@mnma.ac.tz
Mahali : Kivukoni Dar-es-salaam